2 Wafalme 21:19-23
19
Amoni alikuwa na miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka miwili. Mamaye aliitwa Meshulemethi binti Haruzi, kutoka Yotba.
20
Akatenda maovu machoni mwa Bwana, kama baba yake Manase alivyofanya.
21
Akaenenda katika njia zote za baba yake, akaabudu sanamu ambazo baba yake aliziabudu na kuzisujudia.
22
Akamwacha Bwana, Mungu wa baba zake, wala hakuenenda katika njia za Bwana.
23
Watumishi wa Amoni wakafanya fitina juu yake, nao wakamuulia kwake nyumbani.
Settings