Skip to content
1 Samweli 4:7-8

1 Samweli 4:7-8

7
Wafilisti wakaogopa, wakasema, “Mungu amekuja kambini, ole wetu. Halijatokea jambo kama hili tangu hapo.
8
Ole wetu! Ni nani atakayetuokoa kutoka mikononi mwa miungu hii yenye nguvu? Ni miungu ile iliyowapiga Wamisri kwa mapigo ya aina zote huko jangwani.

See also

Where else Scripture says this.

  • Kumbukumbu 32:30

    Mtu mmoja angewezaje kufukuza elfu moja, au wawili kufukuza elfu kumi, kama si kwamba Mwamba wao amewauza, kama si kwamba Bwana amewaacha?
    from verse 7
  • Kutoka 14:25

    Mungu akayaondoa magurudumu ya magari yao, kwa hivyo wakayaendesha kwa shida. Nao Wamisri wakasema, “Tuachane na Waisraeli! Bwana anawapigania dhidi ya Misri.”
    from verse 7
  • Kutoka 15:14

    Mataifa watasikia na kutetemeka, uchungu utawakamata watu wa Ufilisti.
    from verse 7
  • Kutoka 15:16

    vitisho na hofu vitawaangukia. Kwa nguvu ya mkono wako watatulia kama jiwe, mpaka watu wako waishe kupita, Ee Bwana, mpaka watu uliowanunua wapite.
    from verse 7
  • Kutoka 7:5

    Nao Wamisri watajua kuwa Mimi ndimi Bwana nitakapounyoosha mkono wangu dhidi ya Misri na kuwatoa Waisraeli watoke humo.”
    from verse 8
  • Kutoka 9:14

    au wakati huu nitaleta mapigo yangu yenye nguvu dhidi yako, maafisa wako na watu wako, ili upate kujua kuwa hakuna mwingine kama Mimi katika dunia yote.
    from verse 8
  • Zaburi 78:43

    siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
    from verse 8
  • Zaburi 78:51

    Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
    from verse 8

Where this happens

Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options