1 Wafalme 8:54-55
54
Wakati Solomoni alipomaliza dua hizi zote na maombi kwa Bwana, akainuka kutoka mbele ya madhabahu ya Bwana, mahali alipokuwa amepiga magoti, mikono yake ikawa imekunjuliwa kuelekea juu mbinguni.
55
Akasimama na kubariki kusanyiko lote la Israeli kwa sauti kubwa akisema: