Μετάβαση στο περιεχόμενο
1 Wafalme 8:38-40

1 Wafalme 8:38-40

38
wakati dua au maombi yatakapofanywa na mmojawapo wa watu wako Israeli, kila mmoja akitambua taabu za moyo wake mwenyewe, naye akainyoosha mikono yake kuelekea Hekalu hili:
39
basi usikie kutoka mbinguni, katika makao yako. Usamehe na utende, umpe kila mtu kulingana na matendo yake, kwa kuwa unaujua moyo wake (kwa kuwa ni wewe peke yako ujuaye mioyo ya watu wote),
40
ili wakuogope kwa wakati wote watakaoishi katika nchi uliyowapa baba zetu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options