1 Yohana 2:9-11
9
Yeyote anayesema yumo nuruni lakini anamchukia ndugu yake bado yuko gizani.
10
Yeye ampendaye ndugu yake anakaa nuruni, wala hakuna kitu chochote ndani yake cha kumkwaza.
11
Lakini yeyote amchukiaye ndugu yake, yuko gizani na anaenenda gizani, wala hajui anakokwenda, kwa sababu giza limempofusha macho.
Settings