1 Yohana 2:3-6
3
Basi katika hili twajua ya kuwa tumemjua, tukizishika amri zake.
4
Mtu yeyote asemaye kuwa, “Ninamjua,” lakini hazishiki amri zake, ni mwongo, wala ndani ya mtu huyo hamna kweli.
5
Lakini mtu yeyote anayelitii neno lake, upendo wa Mungu umekamilika ndani yake kweli kweli. Katika hili twajua kuwa tumo ndani yake.
6
Yeyote anayesema anakaa ndani yake hana budi kuenenda kama Yesu alivyoenenda.
Settings