1 Wakorintho 15:36-38
36
Ninyi wapumbavu kiasi gani? Mpandacho hakiwi hai kama hakikufa.
37
Mpandapo, hampandi mwili ule utakao kuwa, bali mwapanda mbegu tu, pengine ya ngano au ya kitu kingine.
38
Lakini Mungu huipa mbegu umbo kama alivyokusudia mwenyewe na kila aina ya mbegu huipa umbo lake.