Zaburi93
Listen to this chapter
0:00
0:00
1
Bwana anatawala, amejivika utukufu; Bwana amejivika utukufu tena amejivika nguvu. Dunia imewekwa imara, haitaondoshwa.
2
Kiti chako cha enzi kimekuwa thabiti tangu zamani; wewe umekuwako tangu milele.
3
Bahari zimeinua, Ee Bwana, bahari zimeinua sauti zake; bahari zimeinua sauti za mawimbi yake.
4
Yeye ni mkuu kuliko ngurumo ya maji makuu, ni mkuu kuliko mawimbi ya bahari: Bwana aishiye juu sana ni mkuu.
5
Ee Bwana, sheria zako ni imara; utakatifu umepamba nyumba yako pasipo mwisho.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Options
Study Note