Zaburi150
Listen to this chapter
0:00
0:00
1
Msifuni Bwana. Msifuni Mungu katika patakatifu pake, msifuni katika mbingu zake kuu.
2
Msifuni kwa matendo yake makuu, msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.
3
Msifuni kwa mvumo wa tarumbeta, msifuni kwa kinubi na zeze,
4
msifuni kwa matari na kucheza, msifuni kwa kinanda cha nyuzi na filimbi,
5
msifuni kwa matoazi yaliayo, msifuni kwa matoazi yavumayo sana.
6
Kila chenye pumzi na kimsifu Bwana. Msifuni Bwana!
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Options
Study Note