Skip to content

Zaburi150

1
Msifuni Bwana. Msifuni Mungu katika patakatifu pake, msifuni katika mbingu zake kuu.
2
Msifuni kwa matendo yake makuu, msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.
3
Msifuni kwa mvumo wa tarumbeta, msifuni kwa kinubi na zeze,
4
msifuni kwa matari na kucheza, msifuni kwa kinanda cha nyuzi na filimbi,
5
msifuni kwa matoazi yaliayo, msifuni kwa matoazi yavumayo sana.
6
Kila chenye pumzi na kimsifu Bwana. Msifuni Bwana!
Use arrow keys to navigate
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options